SIFA ZA MALENGO

 *SIFA ZA MALENGO*


1. Yawe wazi yaani yaweze kueleweka kwa wepesi

2. Malengo yanatakiwa kuandikwa 

-Usiweke malengo kichwani peke yake fanya kuandika malengo yako..


3. Yawe na uhalisia 

 - Usiweke malengo nje ya uhalisia.

-Usiweke malengo ya mauzo ya 100M kwa mataji wa 10K.


4. Yaweze kupimika

-Usiweke malengo ambayo hayawezi kupimika kwa mda husika.


5. Malengo yategemee na hali ya sasa.

- Usiweke malengo nje ya uhakisia wako wa sasa.


6. Yawe na mda maalumu.

- Usiweke malengo yasiyo na mda maalumu. Inaweza kuwa mwaka/mwezi.


7. Weka malengo ambayo yanaweza kutekelezeka.

- Usiweke malengo magumu sana mpka unaogopa kutekeleza.


8. Malengo hayatakiwi kuwa mengi mpka yakuvuruge.

- Utakuta mtu ana malengo mengi mpaka yana mvuruga.


9. Jitaidi malengo yako yakite sehemu nyeti kwenye biashara yak.

- Mfano sasa unataka ufike mauzo ya (3,000,000) kwa mwezi (3M) je utafanyaje?

- Tumia mbinu- Zingatia kanuni 80/20 rule

- Gawanya mauzo 3M kwa siku 30 kwa siku ni mauzo ya 100,000 (Laki moja)


- Gawanya laki 1 kwa masaa ya kazi kwenye biashara yako.

Mfano: msaa ya kazi yakiwa 12 basi utahitajika kuuza 8,500 kwa saa...


Tambua idadi ya wateja wako ambao wanaweza kufika hayo mauzo kwa siku.

- Usifanye biashara mpaka ufike mauzo yako kwa siku

-fanya hivyo kila siku bila kuchoka kanuni ya 80/20 rule inasema hivi

 80% ya mauzo ya laki moja yanatakiwa yatokee kwenye 20% ya wateja 


Mfn; Ikiwa wateja 10 wanaweza kukupa mauzo ya laki kwa siku basi kanuni ya 80/20 itakuwa hivi - wateja 2 waweze kukupa 80,000/=


Kwenye biashara unatakiwa kuzingatia wateja wenye hela nyingi kwa wingi usisahau kuweka malengo yako sawa sawa.

Comments

Popular posts from this blog

Jinsi ya kumfanya mwenzi wako akupende zaidi kwa limbwata rahisi tu

NAMNA YA UMASIKINI UNAVYOTENGEZWA

WAJUWE WAGOMBEA WA URAISI WA MAREKANI WALIO GOMBEA WAKIWA GEREZANI